Bomu lalipuka Zanzibar,mmoja afa saba wajeruhiwa

 

Zanzibar, Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Muhamed Khatib Mkombalaguha amefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa vibaya baada ya kurushiwa bomu na watu wasiojulikana.
Tukio hilo limetokea katika eneo la Darajani muda mfupi baada ya maelfu ya wakazi wa zanzibar kuhudhuria mawaidha yaliyokuwa yakitolewa na Sheikh Kassim Mafuta Kassim mkazi wa Pongwe Mkoani Tanga.
Taarifa rasmi kutoka kwa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai Zanzibar (DDCI) Yusuph Ilembo  zimefafanua kuwa Tukio hilo limetokea majira ya saa mbili na nusu usiku wa kuamkia leo na bomu hilo lilirushwa kwa mkono na watu wasiojulikana wakati waumini wakiagana na mtoa mawaidha Sheikh Kassim katika eneo la kuegesha magari Darajani visiwani Zanzibar.
DDCI Ilembo pamoja na kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo amesema jeshi la polisi tayari limeanzisha operesheni maalum ya kuwasaka watu waliohusika na shambulio hilo kwa kushirikiana na vikosi vingine vya ulinzi na usalama visiwani hapa.
“Mlipuko huu pia umesababisha gari mbili zilizokuwepo katika eneo la tukio kuathirika, tumeanza kufanya uchunguzi ingawa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa hadi hivi sasa “ alisema DDCI Ilembo.



 


First

 

Zanzibar, Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Muhamed Khatib Mkombalaguha amefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa vibaya baada ya kurushiwa bomu na watu wasiojulikana.
Tukio hilo limetokea katika eneo la Darajani muda mfupi baada ya maelfu ya wakazi wa zanzibar kuhudhuria mawaidha yaliyokuwa yakitolewa na Sheikh Kassim Mafuta Kassim mkazi wa Pongwe Mkoani Tanga.
Taarifa rasmi kutoka kwa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai Zanzibar (DDCI) Yusuph Ilembo  zimefafanua kuwa Tukio hilo limetokea majira ya saa mbili na nusu usiku wa kuamkia leo na bomu hilo lilirushwa kwa mkono na watu wasiojulikana wakati waumini wakiagana na mtoa mawaidha Sheikh Kassim katika eneo la kuegesha magari Darajani visiwani Zanzibar.
DDCI Ilembo pamoja na kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo amesema jeshi la polisi tayari limeanzisha operesheni maalum ya kuwasaka watu waliohusika na shambulio hilo kwa kushirikiana na vikosi vingine vya ulinzi na usalama visiwani hapa.
“Mlipuko huu pia umesababisha gari mbili zilizokuwepo katika eneo la tukio kuathirika, tumeanza kufanya uchunguzi ingawa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa hadi hivi sasa “ alisema DDCI Ilembo.



 


Next
Newer Post
Previous
This is the last post.