Imam Mohamed Iddriss auwawa Kenya.



Watu wenye silaha wamemuuwa kiongozi wa kiislam Mombasa akiwa ni kiongozi wanne wa kidini kuuwawa mjini humo  katika  miaka miwili iliyopita.

Polisi wanasema  sheikh Mohamed Iddriss mwenyekiti wa baraza la Maiman  na Wahubiri Kenya alipigwa risasi na kuuwawa nje ya msikiti jumanne asubuhi.

Hakuna aliyedai kuhusika na mauaji hayo. Wachunguzi wanasema sheikh  huyo mwenye msimamo wa kadri ametishiwa mara kadhaa na vijana wa kiislam wenye msimamo mkali na alikuwa  na wasi wasi  juu ya maisha yake.

Viongozi watatu wa kiislam waliouwawa  mapema  katika mji huo walishutumiwa kwa kuwa na mahusiano na kundi la alshabab lenye mahusiano na alqaeda lililopo Somalia.

Vikosi vya kijeshi vya Kenya viko Somalia vikipambana na wanamgambo wa Somalia ambao wamekuwa wakifanya mashambulizi Kenya hasa lililokuwa kubwa sana la maduka ya kifahari ya westgate huko Nairobi mwaka jana ambapo zaidi ya watu 60 waliuwawa.

Related Posts



Watu wenye silaha wamemuuwa kiongozi wa kiislam Mombasa akiwa ni kiongozi wanne wa kidini kuuwawa mjini humo  katika  miaka miwili iliyopita.

Polisi wanasema  sheikh Mohamed Iddriss mwenyekiti wa baraza la Maiman  na Wahubiri Kenya alipigwa risasi na kuuwawa nje ya msikiti jumanne asubuhi.

Hakuna aliyedai kuhusika na mauaji hayo. Wachunguzi wanasema sheikh  huyo mwenye msimamo wa kadri ametishiwa mara kadhaa na vijana wa kiislam wenye msimamo mkali na alikuwa  na wasi wasi  juu ya maisha yake.

Viongozi watatu wa kiislam waliouwawa  mapema  katika mji huo walishutumiwa kwa kuwa na mahusiano na kundi la alshabab lenye mahusiano na alqaeda lililopo Somalia.

Vikosi vya kijeshi vya Kenya viko Somalia vikipambana na wanamgambo wa Somalia ambao wamekuwa wakifanya mashambulizi Kenya hasa lililokuwa kubwa sana la maduka ya kifahari ya westgate huko Nairobi mwaka jana ambapo zaidi ya watu 60 waliuwawa.